Programu hii imeandaliwa na Shirika kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi wa Kidato cha Kwanza na Kidato cha Tatu kuimarisha uelewa wao wa masomo katika kipindi cha likizo.
Masomo yatakayofundishwa:
🔻Kiswahili
🔺English
🔻Business Studies
🔺Geography
Muda wa Programu:
Kuanzia tarehe 28/03/2026 hadi 06/04/2026
(Siku za mafunzo ni Jumatatu hadi Jumamosi)
Muda wa Mafunzo kwa Siku:
Saa 08:00 asubuhi hadi saa 13:00 mchana
Mahali:
Shule ya Sekondari Excellence, karibu na Jengo la East Africa, Ubungo Maziwa.
Ada ya Mafunzo:
Tsh 5,000 tu kwa mwanafunzi.
Sheria na Masharti ya Mwanafunzi:
🔺Mwanafunzi azingatie taratibu za programu na shule kwa ujumla.
🔺Mwanafunzi avae mavazi ya heshima na yenye kukubalika katika jamii.
🔺Mwanafunzi awe na madaftari mawili ya msomi kwa ajili ya masomo.
🔺Mwanafunzi awe tayari kusoma kwa bidii na kufuata maelekezo ya walimu.
Wazazi na walezi mnakaribishwa kuwaleta wanafunzi wenu ili wanufaike na programu hii ya elimu.
Mawasiliano: +255758551490, 0679755863, +255618002607 & 0741704992
Karibu Sana!
FANYA USAJILI WA MWANAFUNZI KUPITIA LINK HII.

No comments:
Post a Comment